Taarifa hiyo imebaini kuwa kuwa, viongozi wa Bahrain wanapaswa kusitisha haraka iwezekanavyo vitendo vya kuwakandamiza raia wanaoukosoa na kuupinga utawala wa nchi hiyo. Amnesty International imeongeza kuwa hadi kufikia sasa utawala wa Bahrain umewatia mbaroni au kuwaita na kuwahoji waandamanaji wengi na wanazuoni wa Kishia wasiopungua 60.
Bahrain imekuwa ikishuhudia maandamano ya amani ya wananchi dhidi ya utawala wa Aal Khalifa tangu mwezi Februari mwaka 2011. Wananchi wa Bahrain nwanataka marekebisho ya kisaisa, wanadai ikuwa huru, wanatka kutekelezwa uadilifu, kukomeshwa vitendo vya ubaguzi na kuingia madarakani serikali iliyochaguliwa kwa njia ya kidemokrasia, hata hivyo utawala wa Aal Khalifa siku zote umekuwa ukiwakandamiza raia, kuwaua na kuzuia maandamano ya amani ya raia hao.