Lakini baadhi ya wafasiri wa Qur’ani kama Tabari, wanapofasiri Aya ya 185 ya Surah Al-Baqarah, “Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur'ani kuwa ni uwongofu kwa watu, na hoja zilizo wazi za uwongofu na upambanuzi...”, wamemnukuu Mujahid bin Jabar akisema kuwa Ramadhani inaelekea kuwa ni miongoni mwa majina ya Mwenyezi Mungu na haihusiani na joto kali.
Pia kuna maoni mengine kuhusu jina la Ramadhani, huku wengine wakisema linatoka kwa Ramada as-Sa’im, kumaanisha wakati ambapo mfungaji anahisi joto katika mwili wake kutokana na kiu kali. Wengine wanasema Ramadhani inatoka kwa Armadh, ambayo ina maana ya kushika moto, kama dhambi zinawaka na kuharibiwa na matendo mema.
Wengine wanasema Ramadhani inatokana na Ramadha, ambayo ina maana ya jiwe la moto, huku mioyo ikiyeyuka kwa kutafakari akhera.
Wengine wanasema inatoka kwa Ramdhat an-Nasl, ambayo ina maana ya kunoa upanga, kwani Waarabu walinoa panga zao katika Ramadhani ili kwenda vitani kabla ya miezi ya Haram (wakati vita vilikatazwa).
Katika zama za Jahiliyah (kabla ya kuja Uislamu) mwezi huu uliitwa Natiq na Waarabu waliuheshimu. Watu wa Thamud waliiita Dimmir na mwaka wao ulianza na mwezi huu.
3487543