Kwa mujibu wa taarifa mashindano hayo yamefadhiliwa na yanasimamiwa na Wizara ya Masuala ya Kiislamu ya Saudia kwa ushirikino na Wizara ya Masuala ya Kiislamu ya Mauritania.
Waziri wa Masuala ya Kiislamu Saudia Sheikh Abdullatif Al Al-Sheikh amesema mashindano hayo yatafanyika robo ya kwanza yam waka 1444 Hijria Qamaria. Aidha amebaini kuwa lengo la mashindano hayo ni kuimarisha uhusianoa na ushirikiano katika sekta zote kwa maslahi ya Uislamu na Waislamu.
Jamhuri ya Kiislamu ya Mauritania ni nchi iliyo katika eneo la Maghreb magharibi-kaskazini mwa Afrika.
Idadi ya watu nchini humo inakadiriwa kuwa ni milioni nne na karibu Wamauritania wote ni Waislamu. Harakati za Qur’ani ni mashuhuri katika nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika.
3479243