Msemaji wa OHCHR Marta Hurtado alisema Jumatatu kwamba ingawa chombo cha Umoja wa Mataifa hakikuwa katika nafasi ya kutoa maoni kwa kina kutokana na kutokuwepo kwa taarifa juu ya uamuzi wa Ufaransa na mipango ya utekelezaji, "ni vyema kukumbuka kuwa kulingana na viwango vya kimataifa vya haki za binadamu, vikwazo kuhusu udhihirisho wa dini au imani, ikiwa ni pamoja na uchaguzi wa mavazi, yaliruhusiwa tu katika hali ndogo sana - ikiwa ni pamoja na usalama wa umma, utulivu wa umma, na afya ya umma au maadili."
"Kwa kuongeza, chini ya sheria ya kimataifa ya haki za binadamu, hatua zilizopitishwa kwa jina la utulivu wa umma lazima ziwe sahihi, muhimu na zenye uwiano," aliongeza.
"Jambo jingine lilikuwa kwamba kufikia usawa wa kijinsia kulihitaji kuelewa vikwazo vilivyowazuia wanawake na wasichana kufanya uchaguzi huru, na kuunda mazingira ambayo yanaunga mkono maamuzi yao wenyewe, ikiwa ni pamoja na lakini sio tu katika uchaguzi wa mavazi."
Siku ya Jumapili, Waziri wa Elimu wa Ufaransa Gabriel Attal aliambia kituo cha TV cha TF1 kwamba kuvaa abaya hakutaruhusiwa tena shuleni.
Abaya ni vazi refu linalotiririka kama joho linalovaliwa na wanawake wengi wa Kiislamu. Vazi la abaya ambalo linachukuliwa kuwa buibui la mtindo wa kisasa huvaliwa na baadhi ya wanawake wa Kiislamu kama stara.
Waziri wa Elimu wa Ufaransa Gabriel Attal amesema kuwa, serikali ya nchi hiyo itapiga marufuku wanafunzi kuvaa abaya wakati wanapokuwa shule.
Katika mahojiano na shirika la habari la Ufaransa la TF1, waziri huyo ameeleza kuwa atafanya mazungumzo mapema wiki hii na wakuu wa shule za umma ili kuwasaidia kutekeleza marufuku hiyo.
Marufuku hiyo inatarajiwa kuanza kutekelezwa pindi tu muhula mpya wa masomo utakapoanza mnamo Jumatatu ijayo.
3484985