Polisi wa Toronto wanajaribu kumtambua mtu anayesakwa katika vitendo viwili vya uharibifu katika msikiti wa mashariki. Huko kanada.
Polisi walisema mwanamume huyo aliacha maandishi ya chuki mbele ya msikiti katika eneo la Danforth Avenue na Donlands Avenue.
Polisi walipokea simu Alhamisi kabla ya saa 1 jioni kwa kosa linalotokana na chuki, Mshukiwa anadaiwa kuchora alama za chuki kwenye msikiti wa Madinah Masjid.
Mwanamume huyo anaaminika kuwa mshukiwa yuleyule aliyehusika na tukio jingine la uharibifu lililotokea Ijumaa iliyopita saa 7:30 mchana.
Toronto ilizindua Kampeni ya Kupambana na Kuongezeka kwa chuki dhidi ya Uislamu,
Polisi wamethibitisha kuwa msikiti huo huo uliharibiwa katika matukio yote mawili.
Mwanamume huyo alielezewa kuwa na umri wa miaka 30, mwenye nywele fupi.
Alikuwa amevalia kofia nyeusi ya besiboli, koti jeusi lenye mabaka kwenye mikono, suruali nyeusi na buti nyeusi, polisi walisema.