Ayatullah Kadhim Seddiqi amesema katika hotuba za Swala ya leo ya Ijumaa kwamba: "Shahid Qasem Soleimani aliwaunganisha pamoja kama minyororo mmoja watetezi wa Haram Tukufu kutoka Yemen, Lebanon, Afghanistan, Pakistan, Iraq, Iran na watu huru kote duniani kwa ajili ya kulinda matukufu na akabuni njia mpya ya mapambano.
Ayatullah Seddiqi ameongeza kuwa: “Licha ya mawazo ya rais wa zamani wa Marekani, Donald Trump muuaji na mhalifu habithi na mahabithi wenzake, waliofanya jinai hiyo kwa amri yake wakidhani kwamba mapambano ya Jihadi yangedhoofika kwa kumuua kigaidi Shahidi Soleimani, Wamarekani hawatakuwa na utulivu hata siku moja katika eneo hili."
Khatibu wa Sala ya Ijumaa ya Tehran pia amesema: Wamarekani waliondoka Afghanistan kwa fedheha baada ya kuuawa shahidi Kamanda Soleimani.
Ayatullah Seddiqi ameongeza kuwa: "Adui anayeonekana kuwa na nguvu katika masuala ya silaha, aliyeshindwa kisiasa, kijamii, kimaadili na kimataifa, alikumbana na pigo hilo kali na sasa haweza kufanya kosa lolote."
Vilevile ameashiria nafasi na sifa aali za Bibi Fatimatu Zahra (as), binti kipenzi wa Mtume wetu Muhammad (saw) aliyekufa shahidi siku kama ya jana tarehe 3 Jamadithani na kusema: Bibi Fatima alikusanya pamoja sifa zote njema na kuakisi kivitendo jamali na utukufu wa Mwenyezi Mungu SWT.