Sheikh Naim Qassim sambamba na kuashiria kwamba, hivi sasa eneo la Asia Magharibi linaelekea upande wa amani na uthabiti ameyasifu makubaliano ya Iran na Saudia yaliyofikiwa kwa upatanishi wa China.
Naibu Katibu Mkuu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon ameisifu hatua hiyo ya Iran na Saudia na kubainisha kwamba, makubaliano hayo yamefikiwa kwa kuwa Riyadh na Tehran zinataka kushirikiana baina yao na kuweka muongozo wao kwa ajili ya kuleta uthabiti wa kisiasa wa nchi zao na eneo hili la Asia Magharibi.
Aidha ameongeza kuwa, kile kilichofikiwa baina ya Iran na Saudia kimebadilisha muelekeo wa Asia Magharibi na kwa mara nyingine tena utawala haramu wa Israel umekuwa adui wa kweli wa watu wote.
4135528